Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Matendo 11:7-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Matendo 11:7-12 in Biblia Takatifu

7 Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
Matendo 11 in Biblia Takatifu

Matendo ya Mitume 11:7-12 in Biblia ya Kiswahili

7 Kisha nikasikia sauti ikisema nami, “Amka, Petro, chinja naj ule!”
8 Nikasema, “Siyo hivyo, Bwana, mdomoni mwangu hakujawahi kuingia kitu chochote kisicho kitakatifu au kichafu”
9 Lakini sauti ikajibu tena kutoka Mbinguni, kile Mungu alichokitangaza kuwa ni safi, usikiite najisi,
10 Hii ilitokea mara tatu, na kila kitu kikachukuliwa mbinguni tena.
11 Tazama, wakati huo watu watatu walikuwa wamesimama mbele ya nyumba ile tulimokuwa; wametumwa kutoka Kaisaria kuja kwangu.
12 Roho akaniambia kwenda nao, na nisitofautiane nao. Hawa wanaume sita wakaenda pamoja na mimi na tuliende kwenye nyumba ya mtu mmoja.
Matendo ya Mitume 11 in Biblia ya Kiswahili