Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Matendo - Matendo 10

Matendo 10:9-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
10Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
11Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
13Akasikia sauti ikimwambia: “Petro, amka uchinje, ule!”
14Petro akajibu, “La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu.”
15Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: “Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!”
16Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.

Read Matendo 10Matendo 10
Compare Matendo 10:9-16Matendo 10:9-16