11Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
12Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
13Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
14mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
15kila aina ya kunguru,
16kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
17Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
18bundi mweupe na mwari,
19korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
20Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
21Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
22Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
23Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
24Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.