Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Mambo ya Walawi 11:11-24 in Swahili (individual language)

Help us?

Mambo ya Walawi 11:11-24 in Biblia ya Kiswahili

11 Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
12 Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
13 Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
14 mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
15 kila aina ya kunguru,
16 kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
17 Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
18 bundi mweupe na mwari,
19 korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
20 Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
21 Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
22 Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
23 Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
24 Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
Mambo ya Walawi 11 in Biblia ya Kiswahili