Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Luka 24:36-52 in Swahili (individual language)

Help us?

Luka 24:36-52 in Biblia Takatifu

36 Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia “Amani kwenu.”
37 Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
38 Lakini yeye akawaambia, “Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
39 Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo.”
40 Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
41 Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, “Mnacho chakula chochote hapa?”
42 Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
43 Akakichukua, akala, wote wakimwona.
44 Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”
45 Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
46 Akawaambia, “Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
47 na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
49 Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu.”
50 Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
51 Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
52 Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
Luka 24 in Biblia Takatifu

Luka 24:36-52 in Biblia ya Kiswahili

36 Wakati wakiongea mambo hayo, Yesu mwenyewe alisimama katikati yao, na akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
37 Lakini waliogopa na kujawa na hofu, na wakafikiri kwamba waliona roho.
38 Yesu akawaambia, Kwanini mnafadhaika? Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?
39 Angalieni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe. Niguseni na muone. Kwa maana roho haina nyama na mifupa, kama mnionavyo mimi kuwa navyo.”
40 Alipokwisha kusema hivi, akawaonyesha mikono yake na miguu yake.
41 Walipokuwa bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini, na kustaajabu, Yesu akawaambia, “Je mna kitu chochote cha kula?”
42 Wakampa kipande cha samaki aliyechomwa.
43 Yesu akakichukua, na kukila mbele yao.
44 Akawaambia, “Nilipokuwa nanyi, niliwaambia kwamba yote yalioandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na Zaburi lazima yatimilike.”
45 Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.
46 Akawaambia, “Kwamba imeandikwa, Kristo lazima ateseke, na kufufuka tena kutoka katika wafu siku ya tatu.
47 Na toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe kwa jina lake kwa mataifa yote, kuanzia kutokea Yerusalemu.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
49 Angalia, nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu. Lakini subirini hapa jijini, mpaka mtakapovishwa nguvu kutoka juu.
50 Kisha Yesu akawaongoza nje mpaka walipokaribia Bethania. Akainua mikono yake juu, na akawabariki.
51 Ikatokea kwamba, wakati alipokuwa akiwabariki, aliwaacha na akabebwa juu kuelekea mbinguni.
52 Basi wakamwabudu, na kurudi Yerusalemu na furaha kuu.
Luka 24 in Biblia ya Kiswahili