Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 20

Luka 20:24-34

Help us?
Click on verse(s) to share them!
24“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;

Read Luka 20Luka 20
Compare Luka 20:24-34Luka 20:24-34