Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Hesabu 13:7-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Hesabu 13:7-20 in Biblia ya Kiswahili

7 Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8 Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10 kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11 kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13 kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15 kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16 Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
17 Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
18 Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
19 Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
20 Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
Hesabu 13 in Biblia ya Kiswahili