Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 13

Hesabu 13:7-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
17Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
18Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
19Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
20Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.

Read Hesabu 13Hesabu 13
Compare Hesabu 13:7-20Hesabu 13:7-20