1 Yahwe, Ee Mungu ulipaye kisasi, Mungu ulipaye kisasi, utuangazie sisi.
2 Inuka, muhukumu wa nchi, uwape wenye majivuno kile wanachosahili.
3 Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
4 Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
5 Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
6 Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.