1Yahwe, Ee Mungu ulipaye kisasi, Mungu ulipaye kisasi, utuangazie sisi.
2Inuka, muhukumu wa nchi, uwape wenye majivuno kile wanachosahili.
3Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
4Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
5Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
6Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.