Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 92:9-15 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 92:9-15 in Biblia ya Kiswahili

9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
14 Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
15 kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.
Zaburi 92 in Biblia ya Kiswahili