Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 91:2-9 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 91:2-9 in Biblia ya Kiswahili

2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Zaburi 91 in Biblia ya Kiswahili