Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 88:7-17 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 88:7-17 in Biblia ya Kiswahili

7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. Selah
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? Selah
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
Zaburi 88 in Biblia ya Kiswahili