Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 86:3-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 86:3-12 in Biblia ya Kiswahili

3 Unihurumie, Bwana, maana ninakulilia wewe mchana kutwa.
4 Umfurahishe mtumishi wako, maana ni kwako, Bwana, ninaomba.
5 Wewe, Bwana, ni mwema, na uko tayari kusamehe, na huonesha huruma kubwa kwa wale wanao kulilia wewe.
6 Yahwe, sikiliza maombi yangu; sikia sauti ya ombi langu.
7 Katika siku ya shida ninakuita wewe, kwa maana utanijibu.
8 Katikati ya miungu hakuna wa kufananishwa na wewe, Bwana. Hakuna matendo kama matendo yako.
9 Mataifa yote ambayo umeyafanya yatakuja kwako na kusujudu mbele zako, Bwana. nao wataliheshimu jina lako.
10 Kwa kuwa wewe ni mkuu na utendaye mambo ya ajabu; wewe pekee ndiwe Mungu.
11 Unifundishe njia zako, Yahwe. Kisha nitatembea katika kweli yako. Unifanye kukuheshimu wewe.
12 Bwana Mungu wangu, nitakusifu kwa moyo wangu wote; nitalitukuza jina lako milele.
Zaburi 86 in Biblia ya Kiswahili