Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 86

Zaburi 86:3-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Unihurumie, Bwana, maana ninakulilia wewe mchana kutwa.
4Umfurahishe mtumishi wako, maana ni kwako, Bwana, ninaomba.
5Wewe, Bwana, ni mwema, na uko tayari kusamehe, na huonesha huruma kubwa kwa wale wanao kulilia wewe.
6Yahwe, sikiliza maombi yangu; sikia sauti ya ombi langu.
7Katika siku ya shida ninakuita wewe, kwa maana utanijibu.
8Katikati ya miungu hakuna wa kufananishwa na wewe, Bwana. Hakuna matendo kama matendo yako.
9Mataifa yote ambayo umeyafanya yatakuja kwako na kusujudu mbele zako, Bwana. nao wataliheshimu jina lako.
10Kwa kuwa wewe ni mkuu na utendaye mambo ya ajabu; wewe pekee ndiwe Mungu.
11Unifundishe njia zako, Yahwe. Kisha nitatembea katika kweli yako. Unifanye kukuheshimu wewe.
12Bwana Mungu wangu, nitakusifu kwa moyo wangu wote; nitalitukuza jina lako milele.

Read Zaburi 86Zaburi 86
Compare Zaburi 86:3-12Zaburi 86:3-12