Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 80:5-14 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 80:5-14 in Biblia ya Kiswahili

5 Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
6 Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
7 Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
8 Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
9 Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
12 Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
13 Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
14 Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
Zaburi 80 in Biblia ya Kiswahili