Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:52-61 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:52-61 in Biblia ya Kiswahili

52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili