Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:52-61

Help us?
Click on verse(s) to share them!
52Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:52-61Zaburi 78:52-61