Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:32-72 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:32-72 in Biblia ya Kiswahili

32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili