Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:32-72

Help us?
Click on verse(s) to share them!
32Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:32-72Zaburi 78:32-72