Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:10-25 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:10-25 in Biblia ya Kiswahili

10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili