Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:10-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:10-25Zaburi 78:10-25