11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.