Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 69:3-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 69:3-10 in Biblia ya Kiswahili

3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
Zaburi 69 in Biblia ya Kiswahili