Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 69:11-18 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 69:11-18 in Biblia ya Kiswahili

11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Zaburi 69 in Biblia ya Kiswahili