Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 65:1-6 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 65:1-6 in Biblia ya Kiswahili

1 Kwako wewe, Mungu katika Sayuni, sifa zetu za kungoja; viapo vyetu vitaletwa kwako.
2 Wewe usikiaye maombi yetu, miili yote itakuja kwako.
3 Maovu yanatutawala sisi; kama yalivyo makosa yetu, wewe utayasamehe.
4 Amebarikiwa mtu yule ambaye wewe huchagua kumsogeza karibu yako ili kwamba aishi hekaluni mwako. Tutatoshelezwa kwa uzuri wa nyumba yako, hekalu lako takatifu.
5 Katika haki wewe utatujibu sisi kwa kufanya mambo ya ajabu, Mungu wa wokovu wetu; wewe ambaye ni ujasiri wa mwisho wote wa nchi na wa wale walio mbali toka pande za bahari.
6 Kwa manaa ni wewe ndiye uliyeifanya milima imara, wewe ambaye umefungwa mkanda wa uweza.
Zaburi 65 in Biblia ya Kiswahili