Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 58:3-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 58:3-11 in Biblia ya Kiswahili

3 Waovu huenenda katika upotovu hata walipokuwa tumboni; wao wanaenenda katika upotovu tangu kuzaliwa, wakiongea uongo.
4 Sumu yao ni kama sumu ya nyoka; wako kama fira kiziwi azibaye masikio yake,
5 ambaye hasikilizi sauti ya waganga, haijalishi ustadi walio nao.
6 Vunja meno yao midomoni mwao, Mungu; uyatoe meno ya mwana simba, Yahwe.
7 Wayeyuke kama maporomoko ya maji; wafyatuapo mishale yao, iwe kama haina ncha.
8 Wawe kama konokono ambaye huyeyuka na kutoweka, kama mtoto aliye zaliwa kabla ya wakati ambaye hakuona jua.
9 Kabla ya vyungu vyenu kupata joto la kuungua kwa miiba, yeye ataviondosha kwa upepo mkali, miiba ya kijani yote na ile inayoungua.
10 Mwenye haki atafurahia atakapoona kisasi cha Mungu; ataiosha miguu yake kwenye damu ya waovu,
11 hivyo watu watasema, “Hakika kuna tuzo kwa ajili ya mtu wenye haki; hakika kuna Mungu ahukumuye ulimwengu.”
Zaburi 58 in Biblia ya Kiswahili