Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 52:2-8 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 52:2-8 in Biblia ya Kiswahili

2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. Selah
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. Selah
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
Zaburi 52 in Biblia ya Kiswahili