14 Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
15 Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
16 Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
17 Sadaka ya Mungu ni roho iliyovunjika. Wewe, Mungu hautadharau moyo uliopondeka na kujutia.
18 Uitendee mema Sayuni katika nia yako nzuri; uzijenge tena kuta za Yerusalem.