Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 51:1-7 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 51:1-7 in Biblia ya Kiswahili

1 Unirehemu, Mungu, kwa sababu ya uaminifu wa agano lako; kwa ajili ya wingi wa matendo yako ya rehema, uyafute makosa yangu.
2 Unioshe kabisa uovu wangu na unisafishe dhambi zangu.
3 Kwa maana ninayajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yako siku zote.
4 Dhidi yako, wewe pekee, nimetenda dhambi na kufanya uovu mbele ya macho yako; uko sawa usemapo; wewe uko sahahi utoapo hukumu.
5 Tazama, nilizaliwa katika uovu; pindi tu mama yangu aliponibeba mimba, nilikuwa katika dhambi. Tazama, wewe unahitaji uaminifu ndani ya moyo wangu;
6 katika moyo wangu wewe utanifanya niijue hekima.
7 Unisafishe kwa hisopo, nami nitakuwa safi; unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
Zaburi 51 in Biblia ya Kiswahili