Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 40:13-17 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 40:13-17 in Biblia ya Kiswahili

13 Yahwe, tafadhari uniokoe; njoo haraka unisaidie Yahwe.
14 Waaibike na wafedheheke kabisa wanaufuatilia uhai wangu wauondoe. Warudishwe nyuma na wadharaulike, wale wanaofurahia kuniumiza.
15 Waogopeshwe kwa sababu ya aibu yao, wale waniambiao, “Aha, aha!”
16 Bali wale wote wakutafutao wafurahi na kushangilia katika wewe; na kila mmoja apendaye wokovu wako aseme daima, “Asifiwe Yahwe.”
17 Mimi ni maskini na muhitaji; lakini Bwana hunifikiria. Wewe ni msaada wangu nawe huja kuniokoa; usichelewe, Mungu wangu.
Zaburi 40 in Biblia ya Kiswahili