3 Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
4 Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
5 Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
7 Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.