3Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
4Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
5Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
7Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.