Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 37:23-32 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 37:23-32 in Biblia ya Kiswahili

23 Hatua za mwanadamu zinaimarishwa na Yahwe, mtu ambaye njia zake zinakubalika machoni pa Mungu.
24 Ajapojikwaa, hataanguka chini, kwa kuwa Yahwe anamshikilia kwa mkono wake.
25 Nilikuwa kijana na sasa ni mzee; sijawahi kumuona mtu mwenye haki ametelekezwa wala watoto wake kuombaomba mkate.
26 Wakati wote yeye ni mkarimu na hukopesha, nao watoto wake hufanyika baraka.
27 Acha uovu na ufanye yaliyo mema; ndipo utakapokuwa salama milele.
28 Kwa maana Yahwe hupenda haki naye hawaachi wafuasi waaminifu. Wao hutunzwa milele, lakini uzao wa waovu utafutiliwa mabli.
29 Wenye haki watairithi nchi na kuaa huko milele.
30 Mdomo wa mwenye haki huongea hekima na huongeza haki.
31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; miguu yake haitelezi.
32 Mtu mwovu humvizia mwenye haki na kutafuta kumuua.
Zaburi 37 in Biblia ya Kiswahili