23Hatua za mwanadamu zinaimarishwa na Yahwe, mtu ambaye njia zake zinakubalika machoni pa Mungu.
24Ajapojikwaa, hataanguka chini, kwa kuwa Yahwe anamshikilia kwa mkono wake.
25Nilikuwa kijana na sasa ni mzee; sijawahi kumuona mtu mwenye haki ametelekezwa wala watoto wake kuombaomba mkate.
26Wakati wote yeye ni mkarimu na hukopesha, nao watoto wake hufanyika baraka.
27Acha uovu na ufanye yaliyo mema; ndipo utakapokuwa salama milele.
28Kwa maana Yahwe hupenda haki naye hawaachi wafuasi waaminifu. Wao hutunzwa milele, lakini uzao wa waovu utafutiliwa mabli.
29Wenye haki watairithi nchi na kuaa huko milele.
30Mdomo wa mwenye haki huongea hekima na huongeza haki.
31Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; miguu yake haitelezi.
32Mtu mwovu humvizia mwenye haki na kutafuta kumuua.