4 Kwa kuwa maneno ya Mungu ni ya hakika, na kila afanyacho ni haki.
5 Yeye hupenda haki na kutenda kwa haki. Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe.
6 Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa, na nyota zote ziliumbwa kwa pumzi ya mdomo wake.
7 Yeye huyakusanya maji ya baharini kama rundo; naye huiweka bahari katika ghala.
8 Basi ulimwengu wote umwogope Yahwe; wenyeji wote wa ulimwengu wamuhofu yeye.
9 Kwa maana yeye alisema, na ikafanyika; aliamuru, na ikasimama mahali pake.