Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 29:5-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 29:5-10 in Biblia ya Kiswahili

5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
Zaburi 29 in Biblia ya Kiswahili