9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.