Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 140:7-13 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 140:7-13 in Biblia ya Kiswahili

7 Ee Yahwe, Bwana wangu, wewe ni mwenye nguvu uwezaye kuniokoa; hunifunika ngao kichwa changu siku ya vita.
8 Ee Yahwe, usiyatimize matakwa ya waovu; usiruhusu njama zao kufanikiwa. Selah
9 Wale wanao nizunguka huinua vichwa vyao; madhara ya midomo yao wenyewe na yawafunike.
10 Makaa ya moto na yawaangukie; uwatupe motoni, kwenye shimo refu, wasiweze kuinuka tena.
11 Watu wenye ndimi na wasifanywe salama juu ya nchi; na uovu umuwinde kumpiga mtu mwenye vurugu mpaka afe.
12 Ninajua kuwa Yahwe atahukumu kwa haki walioteswa, na kuwa atawapa haki wahitaji.
13 Hakika watu wenye haki watalishukuru jina lako; watu wanyoofu wataishi uweponi mwako.
Zaburi 140 in Biblia ya Kiswahili