Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 132:2-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 132:2-11 in Biblia ya Kiswahili

2 Kumbuka ndiye aliye mwapia Yahwe, aliweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo.
3 Alisema, sitaingia nyumbani mwangu wala sitaenda kitandani mwangu,
4 sitayapa macho yangu usingizi wala kope zangu kupumzika
5 mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yahwe, na maskani kwa ajili ya Shujaa wa Yakobo.”
6 Tazama tulisikia kuhusu hilo katika Efrata; tuliipata katika konde la Yearimu.
7 Tutaingia katika maskani ya Mungu; tutasujudu miguuni pake.
8 Inuka, Ee Yahwe, uje mahali pako pa kupumzika, wewe na sanduku la nguvu zako!
9 Makuhani wako na wavikwe uadilifu; waaminifu wako washangilie.
10 Kwa ajili ya mtumishi wako Daudi, usimuache mfalme wako uliye mpaka mafuta.
11 Yahwe alimwapia Daudi kiapo cha uhakika, kiapo cha uhakika ambacho hatakivunja: “Nitamuweka mmoja wa wazawa wako kwenye kiti chako cha enzi.
Zaburi 132 in Biblia ya Kiswahili