47 Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.
48 Nitaziinulia mikono yangu amri zako, nizipendazo; nitazitafakari sheria zako. ZAYIN.
49 Kumbuka ahadi yako kwa mtumishi wako kwa sababu umenipa tumaini.
50 Hii ni faraja yangu katika mateso: kuwa ahadi yako imeniweka hai.
51 Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
52 Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
53 Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.