Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:36-47 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:36-47 in Biblia ya Kiswahili

36 Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
37 Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
38 Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
39 Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
40 Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
41 Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
42 ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
43 Usiliondoe neno la kweli mdomoni mwangu, maana nimesubiri kwa ajili ya amri zako za haki.
44 Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.
45 Nitaenenda salama, maana ninayatafuta maagizo yako.
46 Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
47 Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili