Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:36-47

Help us?
Click on verse(s) to share them!
36Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
37Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
38Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
39Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
40Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
41Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
42ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
43Usiliondoe neno la kweli mdomoni mwangu, maana nimesubiri kwa ajili ya amri zako za haki.
44Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.
45Nitaenenda salama, maana ninayatafuta maagizo yako.
46Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
47Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:36-47Zaburi 119:36-47