Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:32-42 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:32-42 in Biblia ya Kiswahili

32 Nitakimbia katika njia ya amri zako, kwa sababu wausukuma moyo wangu kufanya hivyo. HE
33 Unifundishe, Yahwe, njia za sheria yako, nami nitazishika hadi mwisho.
34 Unipe uelewa, nami nitazishika sheria zako; nitazitii kwa moyo wangu wote.
35 Uniongoze katika njia ya amri zako, maana ninafurahi kuenenda katika hizo.
36 Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
37 Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
38 Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
39 Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
40 Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
41 Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
42 ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili