Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:32-42

Help us?
Click on verse(s) to share them!
32Nitakimbia katika njia ya amri zako, kwa sababu wausukuma moyo wangu kufanya hivyo. HE
33Unifundishe, Yahwe, njia za sheria yako, nami nitazishika hadi mwisho.
34Unipe uelewa, nami nitazishika sheria zako; nitazitii kwa moyo wangu wote.
35Uniongoze katika njia ya amri zako, maana ninafurahi kuenenda katika hizo.
36Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
37Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
38Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
39Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
40Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
41Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
42ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:32-42Zaburi 119:32-42