Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 9:8-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 9:8-10 in Biblia Takatifu

8 Basi, jirani zake na wale waliokuwa wanajua kwamba hapo awali alikuwa maskini mwombaji, wakasema, “Je, huyu siye yule maskini aliyekuwa akiketi na kuomba?”
9 Baadhi yao wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “La! Ila anafanana naye.” Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, “Ni mimi!”
10 Basi, wakamwuliza, “Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?”
Yohana 9 in Biblia Takatifu

Yohana 9:8-10 in Biblia ya Kiswahili

8 Majirani wa yule mtu na wale waliomuona mwanzo kama mwombaji walisema, Je! huyu siye yule mtu aliyekuwa akikaa na kuomba?” wengine walisema, “Ni yeye.”
9 Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
10 Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
Yohana 9 in Biblia ya Kiswahili