Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 7:40-44 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 7:40-44 in Biblia Takatifu

40 Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
Yohana 7 in Biblia Takatifu

Yohana 7:40-44 in Biblia ya Kiswahili

40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
Yohana 7 in Biblia ya Kiswahili