Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Yohana 5:37-42 in Swahili (individual language)

Help us?

Yohana 5:37-42 in Biblia Takatifu

37 Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake,
38 na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.
39 Ninyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uzima wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia!
40 Hata hivyo, ninyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima.
41 “Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu.
42 Lakini nawajua ninyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.
Yohana 5 in Biblia Takatifu

Yohana 5:37-42 in Biblia ya Kiswahili

37 Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
38 Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
39 Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na
40 hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
41 Sipokei sifa kutoka kwa watu,
42 lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
Yohana 5 in Biblia ya Kiswahili