Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Warumi 7:21-23 in Swahili (individual language)

Help us?

Warumi 7:21-23 in Biblia Takatifu

21 Basi, nimegundua kanuni hii: ninataka kufanya jema, lakini najikuta kwamba lile lililo baya ndilo ninalochagua.
22 Ndani kabisa katika moyo wangu naifurahia sheria ya Mungu.
23 Lakini naona kwamba kuna sheria nyingine inayofanya kazi mwilini mwangu, sheria ambayo inapingana na ile inayokubaliwa na akili yangu. Hiyo inanifanya niwe mtumwa wa sheria ya dhambi ifanyayo kazi mwilini mwangu.
Warumi 7 in Biblia Takatifu

Warumi 7:21-23 in Biblia ya Kiswahili

21 Nimefahama, tena, imo kanuni ndani yangu ya kutaka kutenda lililo jema, lakini uovu hakika umo ndani yangu.
22 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani.
23 Lakini naona kanuni iliyo tofauti katika viungo vya mwili wangu. Inapiga vita dhidi ya kanuni mpya katika akili zangu. Inanifanya mimi mateka kwa kanuni ya dhambi iliyo katika viungo vya mwili wangu.
Warumi 7 in Biblia ya Kiswahili