31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.